Processing...

News Room

TUTATULIZA WATU MIOYO

TUTATULIZA WATU MIOYO
TUTATULIZA WATU MIOYO
TUTATULIZA WATU MIOYO
+4 More Images
TUTATULIZA WATU MIOYO
TUTATULIZA WATU MIOYO
TUTATULIZA WATU MIOYO
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini – KCMC kwa kushirikiana na uongozi wa TANLINK leo umetembelea ofisi za Crown Media zilizopo Mikocheni, Dar es Salaam, na kufanya mazungumzo ya pamoja na uongozi wa taasisi hiyo. Lengo kuu la ziara hii ni kuimarisha ushirikiano katika upande wa mawasiliano na uelimishaji wa umma, ili kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na kwa wakati kuhusu namna bora ya kuchangia ujenzi wa Taasisi ya Moyo ya KCMC. Kupitia jukwaa la vyombo vya habari, Crown Media inatarajiwa kuwa kiungo muhimu katika kufikisha ujumbe huu kwa jamii kwa upana zaidi. Ujenzi wa Taasisi ya Moyo ya KCMC ni mradi muhimu unaolenga kuboresha huduma za matibabu ya moyo nchini, na mafanikio yake yanategemea mshikamano na ushiriki wa wadau wote, ikiwemo wananchi. KCMC inaendelea kuhamasisha jamii kujitokeza kuchangia mradi huu wa kihistoria, kwani kila mchango ni hatua ya kuokoa maisha. https://www.instagram.com/p/DXY-hWliO0k/?igsh=bHhicGh6OGZud3Jp

Related Stories

TANGA KUSHIRIKI UJENZI
2026-04-27 00:00:00

TANGA KUSHIRIKI UJENZI

READ ARTICLE
KCMC 'Ni mazungumzo na wananchi'.
2026-04-24 00:00:00

KCMC 'Ni mazungumzo na wananchi'.

READ ARTICLE
KCMC NA EFM PAMOJA
2026-04-24 00:00:00

KCMC NA EFM PAMOJA

READ ARTICLE

Join the Discussion

× Preview
🫀 CHANGIA JENGO LA MOYO