17-02-2026 13:22:50
•
KCMC
•
1 min read
KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA APONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI KCMC
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe, leo tarehe 17/02/2026 amefanya ziara ya kikazi katika hospitali ya KCMC, ikilenga kukagua utekelezaji wa majukumu na miradi ya maendeleo ya hospitali.
Ziara hiyo ilianza kwa kikao kifupi kilichowakutanisha uongozi wa KCMC, wakuu wa idara na vitengo pamoja na uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro - Mawenzi. Katika kikao hicho, Dkt. Seif alipokea taarifa ya utendaji na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano na uwajibikaji katika kuboresha huduma za afya.
Aidha, alikagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na KCMC, pia alipatawasaa wakutembelea wodi ya watoto wachanga, akipongeza juhudi zinazofanywa katika kuimarisha huduma za mama na mtoto. Ziara hiyo imeendelea kuimarisha ushirikiano kati ya KCMC na Mawenzi katika kutekeleza ilani ya Serikali ya utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
Related News